Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Masha
Mshomba, akifafanua baadhi ya mambo yanayohusiana na Mfuko kwa waandishi wa
habari.
Na CHRISTIAN GAYA
Mfuko
wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) unategemea kuwa na Mkutano Mkuu wa kwanza wa
mwaka wa wadau mbalimbali wa sekta ya hifadhi ya jamii utakafanyika kuanzia
tarehe 29 mpaka 30 Novemba 2017
katika Ukumbi wa Kimataifa wa Simba AICC Arusha. Kauli mbiu ya mkutano huu ni "Mafao ya Fidia: Haki ya Mfanyakazi na
chachu katika kukuza Uchumi wa Viwanda". Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassimu Majaliwa.
Ikumbukwe ya kuwa njia mojawapo
ya wadau wa mifuko ya hifadhi ya jamii ni kufuatilia na kujua utendaji wa
mifuko hii inayosimamiwa na bodi za wadhamini kwa njia ya mikutano mikuu
inayofanyika kila mwaka.
Hivyo hii itakuwa nafasi ya
kipekee na muhimu sana kwa wadau wa Mfuko wa WCF kuhudhuria kwa ajili ya
kuzungumzia mambo muhimu yanayogusa afya
na ustawi wa Mfuko zinazohusiana na taarifa za ukaguzi wa mahesabu za mwaka ili
kujua nafasi, uwezo wa Mfuko kifedha na kutathmini maendeleo na changamoto
zinazoukabili Mfuko na kupokea maoni ya kuboresha huduma za Mfuko na kuondoa
dukuduku miongoni mwa wadau juu ya Mfuko.
Ni wajibu wa bodi ya
wadhamini ya WCF kuhakikisha ya kuwa taarifa za kuwapasha wadau zinawafikia
wadau wa mfuko huu juu ya kufanyika mkutano mkuu wa mwaka kwa muda muafaka. Maswali
ya kujiuliza ni kama vile taarifa hizo zinazotolewa na WCF zina ubora gani na
je zimewafikia wadau wanaohusika kwa muda muafaka?
Kuwawezesha wadau kutekeleza
haki, wajibu na nguvu walizopewa katika mkutano mkuu wa mwaka kama huu
wanatakiwa kuandaliwa mapema kwa muda muafaka na kupewa habari bora na za hali
ya juu na isipofanyika hivyo basi uwezo wa nguvu wa kisheria waliopewa unakuwa
hauna nguvu yeyote kwa wadau.
Na kwa upande mwingine mtu
anaweza kujiuliza ya kwamba chukulia ya kuwa mwanachama amepelekewa habari na
kupata taarifa mapema juu ya kuhudhuria mkutano mkuu wa kwanza na wadau wa WCF.
Je baada ya hapo inafuatiliwa ili kuhakikisha ya kuwa hawa wadau
watakaochaguliwa kuwawakilisha wenzao kwenye mkutano huo watawajibika kama
inavyotakiwa.
Hivyo kwa upande mwingine
unaweza kusema ya kuwa wadau kupatiwa taarifa na bora kwa muda muda muafaka
hiyo haitoshi kabisa kinachotakiwa hapa
ni kwa hali na mali mdau kuwa tayari kujua au kuelewa kilichoandaliwa kwenye
makabrasha ambalo ni jambo linaloonekana kuwa ni tatizo kubwa kwa wanachama na
wadau wengi.
Mtu mwingine anaweza kuwa na
mashaka na kilichopo ndani ya makabrasha kama siyo pambo tu la kuvutia Mfuko kwa
idadi kubwa ya wadau.
Kwa upande mwingine
wanachama mara nyingi wameonekana kuwa ni kundi ambalo halina nguvu kabisa kwa
kusimamia utendaji na uendeshaji wa mifuko ya hifadhi hii ya jamii ikiwemo
kufuatilia tabia na utaratibu wa utendaji wa wadhamini au bodi hizi za hifadhi
ya jamii na hata inaonekana
wanatofautiana katika mitazamo kwa upande mwingine
Hapa ikumbuka kwamba uhai na
ustawi wa mifuko ya hifadhi ya jamii siyo kweli ya kwamba inategemewa na
mikutano mikuu ya mwaka ya mifuko kama huu utakaofanyika huko Arusha na WCF
ingawa ni mojawapo ya mlango muhimu wa ufahamu kama mfuko wa pensheni wa
hifadhi ya jamii.
Wadau wa Mfuko wametawanyika
karibu mikoa yote ya Tanzania kuanzia ngazi za Vitongoji, Vijiji, Wilaya,
Kimkoa na hadi Kitaifa hivyo kwa maana hii inalazimisha kuwepo na uwakilishi
katika kuhudhuria kwenye mkutano mkuu huu wa mwaka.
Kutokana na msambaratiko huu
wa wadau na hatimaye kuwakilishwa na watu wachache kutoka kila kampuni za umma
na za watu binafsi, na taasisi
mbalimbali za serikali kwa hiyo hata mahudhuria ya wadau kwenye mkutano mkuu wa
mwaka umekuwa wa matatizo kwa kuhudhuriwa na wadau wachache wawakilishi. Kwa
sababu hii imesababisa mpaka kuwepo na uwakilishi katika mkutano mkuu wa kila
mwaka badala ya wadau wote kuhudhuria.
Jambo la kujiuliza ni kwamba
je hawa wawakilishi kutoka kwa waajiri mbalimbali wanakutana na wafanyakazi
wenzao au kama ni mwajiri je naye
anahakikishaje kutoa taarifa kwa ukamilifu na ubora ule ule uliotolewa wakati
wa mkutano mkuu wa mwaka wa wadau
Kwa kifupi ni kwamba je
wanachama hupewa taarifa na wawakilishi mara tu baada ya kutoka kwenye
mahudhurio ya mkutano mkuu? Na kama hawapewi kunakuwepo na maana gani ya kuwa
na mwakilishi wa wafanyakazi wenzao?
Hivyo kuna haja ya kuwa na
malengo na mikakati ya makusudi ya kuhakikisha ya kuwa waajiri, wafanyakazi, na
taasisi mbalimbali kuchagua mwakilishi ambaye atakuwa ni mtu ambaye atashiriki
kwa malengo ya kuelewa na kujua mambo muhimu ya mkutano mkuu hasa yanayogusa
uhai, afya na ustawi wa Mfuko kwa malengo ya kuboresha huduma kwa wafanyakazi ambao
wataumia, wataugua ama watafariki kutokana na kazi wanazozifanya kwa mujibu wa
mikataba ya ajira zao.
Mfuko wa WCF ni
Taasisi ya hifadhi ya jamii iliyoundwa kwa mujibu wa kifungu cha 5 cha Sheria ya
Fidia kwa Wafanyakazi (Sura 263 marejeo ya mwaka 2015). Lengo kuu la kuanzishwa kwa Mfuko huu ni kushughulikia
masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi waliopo katika sekta ya umma na binafsi
Tanzania Bara ambao wanaumia, wanaugua ama kufariki kutokana na kazi
wanazozifanya kwa mujibu wa mikataba ya ajira zao
.
Mwandishi
wa makala hii ni mwanzilishi wa Kituo cha HakiPensheni, mshauri na mtaalamu wa
masuala ya pensheni. Kwa maelezo zaidi gayagmc@yahoo.com unaweza kutembelea tovuti hakipensheni
monitor online na hakipensheni blog
Simu +255 655 13 13 41
No comments :
Post a Comment