Tuesday, November 21, 2017

JENGO LA CLOUDS MEDIA GROUP LAUNGUA MOTO


_98841548_screenshot2017-11-21at12.42.11.png
Muonekano wa Jengo la Clouds Media Group.
_98841550_screenshot2017-11-21at12.43.08.png
Mojawapo ya wafanyakazi wa Clouds Media Group akijaribu kuokoa baadhi ya vifaa
7964B80D-C1D0-4CAD-BA38-AEAE652A2A08.jpeg
Magari ya Zimamoto yaliyofika kupambana na moto huo.
…………..
SEHEMU  ya jengo la kituo cha Clouds Media Group lililoko Mikocheni jijini Dar es Salaam limeungua moto leo ambapo Mkurugenzi wa Vipindi wa kituo hicho, Ruge Mutahaba, amesema moto huo ulitokea bila ya mtu yeyote kuwa na taarifa nao ambapo ulianzia katika studio ndogo ya kurekodia.
Aliongeza kwamba kituo hicho si mara ya kwanza kupatwa majanga ya moto ambapo mara ya kwanza walipokuwa katika jengo la Kitegauchumi eneo la Posta jijini Dar es Salaam, moto uliteketeza studio zao na kupoteza vitu mbalimbali ambapo moto wa leo umeteketeza baadhi ya ofisi za studio ya Televisheni.
Hata hivyo, alikishukuru kikosi cha Zimamoto kwa kufika haraka eneo la tukio na kuuzima moto huo.  Vilevile alisema hakuna binadamu aliyepata madhara kutokana na tukio hilo.
Mutahaba alisema juhudi zaidi zinaendelea katika kituo hicho ili kurekebisha mambo yaliyotokea na kwamba ratiba zao zitaendelea kama kawaida.

No comments :

Post a Comment