Muonekano wa Jengo la Clouds Media Group.
Magari ya Zimamoto yaliyofika kupambana na moto huo.
…………..
SEHEMU ya jengo la kituo cha
Clouds Media Group lililoko Mikocheni jijini Dar es Salaam limeungua
moto leo ambapo Mkurugenzi wa Vipindi wa kituo hicho, Ruge Mutahaba,
amesema moto huo ulitokea bila ya mtu yeyote kuwa na taarifa nao ambapo
ulianzia katika studio ndogo ya kurekodia.
Aliongeza kwamba kituo hicho si
mara ya kwanza kupatwa majanga ya moto ambapo mara ya kwanza walipokuwa
katika jengo la Kitegauchumi eneo la Posta jijini Dar es Salaam, moto
uliteketeza studio zao na kupoteza vitu mbalimbali ambapo moto wa leo
umeteketeza baadhi ya ofisi za studio ya Televisheni.
Hata hivyo, alikishukuru kikosi
cha Zimamoto kwa kufika haraka eneo la tukio na kuuzima moto huo.
Vilevile alisema hakuna binadamu aliyepata madhara kutokana na tukio
hilo.
Mutahaba alisema juhudi zaidi
zinaendelea katika kituo hicho ili kurekebisha mambo yaliyotokea na
kwamba ratiba zao zitaendelea kama kawaida.
No comments :
Post a Comment