Mufti Sheikh Abubakari Zubeir bin
Ally akimkabidhi tuzo ya shukrani Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya
Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi wakati wa hafla fupi ya
kumaliza kambi ya siku nne ya upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo
kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa
Cathlab iliyofanywa na Taasisi hiyo kwa kushirikiana na Taasisi ya
Kimataifa ya Kiislamu ya Misaada (IIRO) ya nchini Saudi Arabia. Kushoto
ni Balozi wa Saudi Arabia Nchini Mhe. Mohamed bin Mansour Al Malik.
Balozi wa Saudi Arabia Nchini
Mhe. Mohamed bin Mansour Al Malik akimkabidhi tuzo ya shukrani Mufti
Sheikh Abubakari Zubeir bin Ally katika hafla fupi ya kumaliza kambi ya
siku nne ya upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu
wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab iliyofanywa na
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Taasisi ya
Kimataifa ya Kiislamu ya Misaada (IIRO) ya nchini Saudi Arabia. Jumla
ya wagonjwa 33 walifanyiwa upasuaji katika kambi hiyo.
Kaimu Mkurugenzi wa Tiba kutoka
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Dkt. Doroth Gwajima
akiishukuru Serikali ya Saudi Arabia kupitia Taasisi ya Kimataifa ya
Kiislamu ya Misaada (IIRO) ya nchi hiyo kwa kutuma wataalamu wake hapa
nchini kutoa huduma ya upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia
mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab
iliyofanyika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Jumla ya
wagonjwa 33 walifanyiwa upasuaji katika kambi hiyo.
Madaktari bigwa wa Magonjwa ya
Moyo kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa
Taasisi ya Kimataifa ya Kiislamu ya Misaada (IIRO) ya nchini Saud
Arabia wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza kufanya
upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono
(Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab kwa wagonjwa 33.
No comments :
Post a Comment