Kiongozi
wa msafara wa wawakilishi wa kampuni ya Henan Juren Crane Group kutoka
Jimbo la Henan nchini China, Wang Yuheng (wa pili kulia) akisisitiza
jambo wakati alipokutana na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Ushirika wa
Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (TFC), Bw. Henry Mwatwinza
Mwimbe (kulia). Tukio hili lilifanyika jana, Alhamisi, Novemba 16, 2017
jijini Dar es Salaam.
Na Daniel Mbega
SOMA ZAIDI »
Na Daniel Mbega
WANANCHI
wa mikoa ya Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga na Simiyu wanaweza
kujikwamua kiuchumi kwa kutumia kilimo cha umwagiliaji ifikapo mwaka
2019 kutokana na kuwepo kwa mpango wa uwekezaji unaolenga kuchimbia
visima virefu pamoja na mabwawa katika maeneo mbalimbali nchini
Tanzania.
Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Ushirika wa Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (TFC Ltd), Bw. Henry Mwantwinza Mwimbe, amesema hayo jana baada ya kukutana na wawakilishi wa kampuni ya Henan Juren Group ya China, ambayo imeonyesha nia ya kuwekeza kwa ubia nchini kwa kutengeneza zana mbalimbali za kilimo ikiwa ni pamoja na kuchimba visima katika maeneo yaliyo kame.
Lengo la
uwekezaji huo, kwa mujibu wa Mwimbe, ni kuwakwamua wakulima kiuchumi kwa
kuwa na kilimo endelevu cha umwagiliaji badala ya kutegemea mvua,
ambazo zimekuwa hazina uhakika kwa sababu ya mabadiliko ya tabianchi
yanayotokana na uharibifu wa mazingira.
“Wanachama wetu karibu asilimia 80 wanajihusisha na kilimo, hivyo tunaona itakuwa ni vyema kama tutabadilisha namna ya uendeshaji wa kilimo hiki ili kilete tija kwao na kwa taifa kwa ujumla.
“Katika maeneo mengi mvua zinanyesha mara moja kwa mwaka na wakati mwingine siyo za kutosha, matokeo yake wananchi wanashindwa hata kupata mavuno yanayojidhi matumizi ya nyumbani, achilia mbali ziada ya kuuza sokoni, lakini kilimo cha umwagiliaji kina uhakika na kinaweza kuendeshwa wakati wote wa mwaka,” alieleza Mwimbe.
Alisema
kwamba bado wapo katika hatua za awali kuhusu mchakato huo na akafafanua
kwamba, mradi huo utawahusisha wanachama wote nchini walio kwenye
ushirika ambao watashirikishwa.
Hata hivyo, alisema mradi mama ni kuunganisha (assembling) zana za kilimo kutoka China kama matrekta na mashine nyingine zinazoendana na kilimo watakazoziuza kwa wakulima wa ndani pamoja na nchi jirani, lakini wanaona kwamba hilo litafanikiwa ikiwa wakulima watajengewa uwezo hasa kwa kuwa na uhakika wa maji ili kuendesha kilimo cha umwagiliaji. Mkalimani, Dkt. Chikira Ismail Msangi, akifasili kuhusu azma ya wawekezaji hao katika kuanzisha kampuni ya ubia itakayounganisha zana za kilimo kama matrekta na mitambo ya uchimbaji visima na umwagiliaji hapa nchini. Kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Ushirika wa Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (TFC), Bw. Henry Mwimbe. Tukio hili lilifanyika jana, Alhamisi, Novemba 16, 2017 jijini Dar es Salaam.
“Vijijini watu wana matrekta lakini yanatumika mara moja tu kwa mwaka kwa sababu ya kutegemea mvua, kwa kutumia kilimo cha umwagiliaji ni wazi kwamba wakulima watahitaji nyenzo zaidi ili kurahisisha kilimo chao, lakini lazima kwanza maji yapatikane.
“Israel ni nchi ya jangwa, lakini leo ukienda imebadilika kutokana na kuwepo kwa visima vilivyochimbwa pamoja na mabwawa na wanalima mazao mengi yenye ubora na kuyasafirisha duniani kote, sisi Tanzania tunayo ardhi ya kutosha ambayo tunashindwa kuitumia kwa kuwa tu mahali pengi hakuna vyanzo vya uhakika vya maji.
“Shinyanga, Simiyu, Tabora, Singida, Dodoma na Manyara ni mikoa ambayo ina shida kubwa ya maji japo ina ardhi kubwa, lakini kama watachimbiwa visima wanaweza kufanya kilimo kwa uhakika na kuwavutia hata vijana wanaokimbilia mijini kutafuta ajira,” alisema.
Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Ushirika wa Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (TFC Ltd), Bw. Henry Mwantwinza Mwimbe, amesema hayo jana baada ya kukutana na wawakilishi wa kampuni ya Henan Juren Group ya China, ambayo imeonyesha nia ya kuwekeza kwa ubia nchini kwa kutengeneza zana mbalimbali za kilimo ikiwa ni pamoja na kuchimba visima katika maeneo yaliyo kame.
“Wanachama wetu karibu asilimia 80 wanajihusisha na kilimo, hivyo tunaona itakuwa ni vyema kama tutabadilisha namna ya uendeshaji wa kilimo hiki ili kilete tija kwao na kwa taifa kwa ujumla.
“Katika maeneo mengi mvua zinanyesha mara moja kwa mwaka na wakati mwingine siyo za kutosha, matokeo yake wananchi wanashindwa hata kupata mavuno yanayojidhi matumizi ya nyumbani, achilia mbali ziada ya kuuza sokoni, lakini kilimo cha umwagiliaji kina uhakika na kinaweza kuendeshwa wakati wote wa mwaka,” alieleza Mwimbe.
Hata hivyo, alisema mradi mama ni kuunganisha (assembling) zana za kilimo kutoka China kama matrekta na mashine nyingine zinazoendana na kilimo watakazoziuza kwa wakulima wa ndani pamoja na nchi jirani, lakini wanaona kwamba hilo litafanikiwa ikiwa wakulima watajengewa uwezo hasa kwa kuwa na uhakika wa maji ili kuendesha kilimo cha umwagiliaji. Mkalimani, Dkt. Chikira Ismail Msangi, akifasili kuhusu azma ya wawekezaji hao katika kuanzisha kampuni ya ubia itakayounganisha zana za kilimo kama matrekta na mitambo ya uchimbaji visima na umwagiliaji hapa nchini. Kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Ushirika wa Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (TFC), Bw. Henry Mwimbe. Tukio hili lilifanyika jana, Alhamisi, Novemba 16, 2017 jijini Dar es Salaam.
“Vijijini watu wana matrekta lakini yanatumika mara moja tu kwa mwaka kwa sababu ya kutegemea mvua, kwa kutumia kilimo cha umwagiliaji ni wazi kwamba wakulima watahitaji nyenzo zaidi ili kurahisisha kilimo chao, lakini lazima kwanza maji yapatikane.
“Israel ni nchi ya jangwa, lakini leo ukienda imebadilika kutokana na kuwepo kwa visima vilivyochimbwa pamoja na mabwawa na wanalima mazao mengi yenye ubora na kuyasafirisha duniani kote, sisi Tanzania tunayo ardhi ya kutosha ambayo tunashindwa kuitumia kwa kuwa tu mahali pengi hakuna vyanzo vya uhakika vya maji.
“Shinyanga, Simiyu, Tabora, Singida, Dodoma na Manyara ni mikoa ambayo ina shida kubwa ya maji japo ina ardhi kubwa, lakini kama watachimbiwa visima wanaweza kufanya kilimo kwa uhakika na kuwavutia hata vijana wanaokimbilia mijini kutafuta ajira,” alisema.
Mwimbe
alisema kwamba, katika maeneo ambayo yana mito na vijito kama ya mikoa
ya Mtwara, Lindi, Ruvuma, Rukwa, Katavi na mingineyo, wanaweza
kuchimbiwa mabwawa makubwa ya kuvuna maji ya mvua ambayo yatatumika
kwenye kilimo cha umwagiliaji wakati wa kiangazi.
Wachina wako tayari Hii ni mitambo itakayounganishwa hapa nchini ambayo ni maalum kwa shughuli za ujenzi na uchimbaji wa mabwawa ya maji. Bw. Henry Mwimbe (kulia) Mkurugenzi wa Maendeleo ya Ushirika wa TFC akionyesha kufurahishwa na picha za mitambo ya uchimbaji mabwawa. Tukio hili lilifanyika jana, Alhamisi, Novemba 16, 2017 jijini Dar es Salaam.
Wachina wako tayari Hii ni mitambo itakayounganishwa hapa nchini ambayo ni maalum kwa shughuli za ujenzi na uchimbaji wa mabwawa ya maji. Bw. Henry Mwimbe (kulia) Mkurugenzi wa Maendeleo ya Ushirika wa TFC akionyesha kufurahishwa na picha za mitambo ya uchimbaji mabwawa. Tukio hili lilifanyika jana, Alhamisi, Novemba 16, 2017 jijini Dar es Salaam.
No comments :
Post a Comment