Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa
na Michezo Mhe.Dkt Harrison Mwakyembe akizungumza na viongozi na
wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA) jana Jijini
Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya miaka 30 ya chama hicho.
Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi
wa Habari Wanawake (TAMWA) Bibi Alack Mayombo akieleza mafanikio ya
chama chao ikiwa ni pamoja na kupambana na ukatili wa kijinsia jana
Jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya miaka 30 ya chama hicho.
Mkurugenzi wa Chama cha
Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA) Bibi Edda Sanga akieleza majukumu
ya chama chao jana Jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya miaka
30 ya chama hicho.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa
na Michezo Mhe.Dkt Harrison Mwakyembe akikata utepe kuashiria uzinduzi
wa kitabu cha mafanikio tangu kuanzishwa kwa Chama cha Waandishi wa
Habari Wanawake (TAMWA) jana Jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho
ya kutimiza miaka 30 ya chama hicho.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa
na Michezo Mhe.Dkt Harrison Mwakyembe akibonyeza kitufe kuashiria
uzinduzi wa luninga ya mtandaoni ya Chama cha Waandishi wa Habari
Wanawake (TAMWA) jana Jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya
kutimiza miaka 30 ya chama hicho. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa
Idara ya Habari Maelezo na Msemaji wa Serikali Dkt. Hassan Abbas.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa
na Michezo Mhe.Dkt Harrison Mwakyembe akimkabidhi Tuzo ya Heshima Bibi
Fatma Alloo kwa mchango wake katika Chama cha Waandishi wa Habari
Wanawake (TAMWA) jana Jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya
kutimiza miaka 30 ya chama hicho.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa
na Michezo Mhe.Dkt Harrison Mwakyembe (katikati) akiwa katika picha ya
pamoja na viongozi na baadhi ya wanachama wa Chama cha Waandishi wa
Habari Wanawake (TAMWA) jana Jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho
ya kutimiza miaka 30 ya chama hicho. Wa pili kulia ni Mkurugenzi wa
Idara ya Habari Maelezo na Msemaji wa Serikali Dkt. Hassan Abbas.
…………………………………………………………………………………..
Na. Shamimu Nyaki –WHUSM.
Waziri wa Habari,Utamaduni Sanaa
na Michezo Mhe Dkt. Harrison Mwakyembe ametoa pongezi kwa Chama cha
Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA) kwa kuwa na wanachama ambao
wanakidhi vigezo vilivyopo katika ...
Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka
2016 ambapo moja ya vigezo hivyo ni kuwa na Wanataaluma ya Habari wenye
elimu ya kuanzia Stashahada.
Waziri Mwakyembe ameyasema hayo
Jana Jijini Dar es Salaam katika sherehe za maadhimisho ya miaka 30 ya
Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA) ambapo amewataka
wanachama hao kuendelea na juhudi zao za kukemea ukatili wa kijinsia,
ndoa za utotoni, na mauaji ya vikongwe yaliyotoa sifa kubwa kwa chama
hicho.
“Nimefurahi sana kusikia kuwa
wanachama wa chama hiki wanaanzia ngazi ya Stashahada kama ambavyo
Sheria yetu ya Habari inavyosema kuwa ni lazima kwa mwanataaluma ya
Habari kuwa na kiwango cha Elimu kinachoanzia hapo,lakini pia Serikali
inatambua sana mchango wenu wa kuilemisha jamii masuala mbalimbali
ikiwemo ukatili wa kijinsia endeleeni kufanya hivyo ili jamii yetu iwe
jamii bora”.Alisema Mhe. Mwakyembe.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa
Chama hicho Bibi Alack Mayombo ameishukuru Serikali kwa mchango mkubwa
inaotoa kwa Chama hicho pindi inapohitaji msaada na kuahidi kushirikiana
na Serikali katika kuelimisha jamii hasa masuala ya Ukatili wa
Kijinsia.
“Tunashukuru sana Serikali kwa
jinsi inavyotuunga mkono katika juhudi zetu za kutatua changamoto
zinazoikumba jamii yetu hasa mauaji ya Vikongwe,watu wenye ulemavu wa
ngozi,ndoa za utotoni pamoja na ukatili wa kijinsia mara zote tulizotoa
taarifa kwa Serikali imekuwa ikichukua hatua zinazostahili”. Aliongeza
Bibi Alack.
Naye Mkurugenzi wa Chama hicho Bi
Edda Sanga ameeleza kuwa kwa kipindi cha miaka 30 tangu kilipoundwa
chama hicho kimefanikiwa kufanya tafiti mbalimbali ikiwemo kiwango cha
Ukeketaji, Mimba za utotoni, madawa ya kulevya na athari zake katika
jamii na kutoa taarifa ambayo imesaidia kupunguza matatizo hayo.
Chama hicho kilianzishwa tarehe
17 Novemba 1987 na wanahabari wanawake lengo ikiwa ni kupinga ukatili wa
aina yoyote katika jamii na tayari kimeefanikiwa kwa kiasi
kikubwa,Aidha chama hicho kimezindua luninga ya Mtandaoni itakayotoa
taarifa mbalimbali za Ukatili wa kijinsia pamoja na mambo mengine ya
kijamii.
No comments :
Post a Comment