NAIBU
Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, (TAKUKURU), Brigedia Jenerali
John Julius Mbungo na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es
Salaam, SACP, Lazaro Mambosasawamesema tayari watu kadhaa {vigogo), waliotajwa
kwenye ripoti ya vito vya almasi na madini mengine, wanashikiliwa na kuhojwia
kuhusiana na uhusika wao kwenye kashfa hiyo.
Viongozi
hao wa vyombo vya dola, wamedokeza kukamatwa kwa vigogo hao, wakati Waziri wa
Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, alipokuwa akipokea ripoti ya kukamatwa kwa
almasi kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam, hivi karibuni.
“Nikuhakikishie
tu Mhe. Waziri, watu wetu wako kazini na hivi sasa tunapozungumza watu kadhaa
wamekwishakamatwa kwa sababu za kiupelelezi, siwezi kutaja majina yao kwa sasa
lakini nikuhakikishie tu kwamba wanahojiwa ili kujua uhusika wao katika sakata
hili na kasha tuandae mashtaka dhidi yao,” alisema Naibu Mkurugenzi Mkuu wa
TAKUKURU.
Naye
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, alisema, licha
ya kuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, pia anamuwakilisha
Mkuu wa Jeshi la Polisi, na kwamba na wao wako kazini na tayari “wamewadaka”
watu kadhaa na wako kwenye mahojiano ili kujua namna walivyoshiriki kwenye
njama ya kushusha thamani ya madini hayo ya Almasi.Madini hayo yalizuiwa kwenye
uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, saa chache kabla ya
kusafirishwa kwenda nje ya nchi.
“Mheshimiwa
Waziri, bila shaka maelekezo haya uliyoyatoa ni maelekezo ya Mhe Rais, kwa
hivyo sisi kama vyombo vya ulinzi na usalama hatutakaa kimya kuvumilia
uyoroshwaji wa mali zetu na hivyo kulifanya taifa kuwa ombaomba kila wakati.”
Aisema, Kamanda Mambosasa.
AwaliWaziri
wa Fedha na Mipango, ambaye alifika uwanjani hapo kukagua madini yaliyozuiwa na
serikali baada ya kugundulika kuwa yalipewa thamani pungufu ya ile halisi.
Waziri
alsiema, taifa limepoteza mamilioni ya dola za kimarekani katika udanganyifu
huo.
“Niwaagize
ninyi vyombo vya ulinzi na usalama, watu wote kuanzia kule mgodini hadi hapa,
walioshiriki au waliokuwa wakishiriki kufanya vitendo hivi watiwe mbaroni,
wachunguzwe na mali zao zikamatwe mara moja,” alisema Dkt. Mpango kwa hasira.
Dkt.
Mpango pia alionya ofisi ya mwendesha mashtaka mkuu wa serikali kutokuwa
uchochoro wa kushindwa kwenye kesi na kwamba ushahidi wote uko wazi.
“Lazima
mali za watanzania zirudi kwa watanzania wenyewe, na sio kwa watu wachache.”
Alisema Dkt.Mpango.
Akijibu maelezo hayo ya Mhe. Waziri, Mkurugenzi wa Mashataka, (DPP), Bw. Biswalo Mganga, alimuhakikishia Waziri Mpango, kuwa wote waliotajwa, kwa mujibu wa sheria, mali zao zitataifishwa kama watapatikana na hatia.
Katika hatua ningine, Waziri Mpango alipata fursa ya kukagua almasi iliyokamatwa na kupewa thamani ya chini ambapo Kamishna wa TRA, Bw. Kichere alsiema, kwa mujibu wa sheria kufanya udanganyifu wa mali chini ya sheria ya forodha ya Afrika Mashariki, mali hiyo inataifishwa na inakuwa mali ya serikali.
Alamsi hiyo inatoka mgodi wa Mwadui mkoani Shinyanga.
Akijibu maelezo hayo ya Mhe. Waziri, Mkurugenzi wa Mashataka, (DPP), Bw. Biswalo Mganga, alimuhakikishia Waziri Mpango, kuwa wote waliotajwa, kwa mujibu wa sheria, mali zao zitataifishwa kama watapatikana na hatia.
Katika hatua ningine, Waziri Mpango alipata fursa ya kukagua almasi iliyokamatwa na kupewa thamani ya chini ambapo Kamishna wa TRA, Bw. Kichere alsiema, kwa mujibu wa sheria kufanya udanganyifu wa mali chini ya sheria ya forodha ya Afrika Mashariki, mali hiyo inataifishwa na inakuwa mali ya serikali.
Alamsi hiyo inatoka mgodi wa Mwadui mkoani Shinyanga.
No comments :
Post a Comment