Na Beatrice Lyimo-MAELEZO, DODOMA
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na
Jamhuri ya Afrika Kusini zaridhia kutekeleza Programu ya Urithi wa
Ukombozi wa Bara la Afrika.
Makubaliano hayo yamefanyika
tarehe 19/09/2017 baina ya Tanzania na Afrika Kusini yakiwahusisha
Mawaziri wenye dhamana ya Utamaduni kutoka nchi hizo pamoja na Mawaziri
kutoka Wizara za kisekta zinazohusika na ...
utekelezaji wa Programu hiyo.
Akizungumza wakati wa kusaini
makubaliano hayo, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt.
Harrison Mwakyembe amesema kuwa Tanzania ina mchango wa hali na mali
katika harakati za ukombozi wa nchi za Bara la Afrika pamoja na
uanzishwaji wa program hiyo inayolenga kuhifadhi Urithi huo kwa
kushirikiana na wadau.
“ Mwaka 2002 programu hiyo
iliridhiwa na Mkutano Mkuu wa 33 wa Shirika la Umoja wa Mataifa la
Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na Mkutano Mkuu wa Umoja wa Afrika
(AU) wa mwezi Januari, 2011” ameongeza Dkt. Mwakyembe.
Aidha, Dkt. Mwakyembe amesema
kuwa, moja ya makubalino ni kuendeleza jitihada za kufanya tafiti zaidi
baada ya kukamilika kwa utafiti wa Mradi wa Hashimu Mbita na kufanya
juhudi za makusudi kuorodhesha nyaraka za iliyokuwa Kamati ya Ukombozi
wa Bara la Afrika katika kumbukumbu ya Dunia.
Kwa upande wake Waziri wa Sanaa na
Utamaduni wa Afrika Kusini Nathi Mthethwa amesema kuwa Programu hiyo
itaimarisha ushirikiano katika kuongeza idadi ya maeneo ya Urithi wa
Dunia yanayohusiana na Harakati za Ukombozi yanaorodheshwa kwa pamoja
baia ya nchi moja na nyingine hususani Urithi wa Ukombozi usioshikika.
“Kuna baadhi ya vizazi havielewi
machungu ya kutawaliwa, hivyo nashauri mifumo ya elimu katika nchi za
Afrika izingatie masuala ya ukombozi wa Bara la Afrika ili kuleta uelewa
kwa kizazi kilichopo na vizazi vijavyo” ameongeza Mhe. Mthethwa.
Programu hiyo ina wajibu wa
kukusanya, kuweka kumbukumbu, kuhifadhi na kukumbuka nakishi ya Urithi
wa Afrika tangu harakati za kupigania Uhuru wa Afrika hadi Bara zima
lilipokombolewa.
No comments :
Post a Comment