Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo
ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi.
Leah Kihimbi akizungumza kwa niaba ya Waziri Dkt. Harrison Mwakyembe
katika mkutano wa wadau katika kuchangia ushiriki wa Tanzania katika
Tamasha la Utamaduni la Afrika Mashariki (Jamafest) leo Jijini Dar es
Salaam. Tanzania inatarajiwa kuwakilishwa na wasanii takribani 240.
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu
Tanzania Bibi. Joyce Fissoo akifafanua jambo wakati katika mkutano wa
wadau katika kuchangia ushiriki wa Tanzania katika Tamasha la Utamaduni
la Afrika Mashariki (Jamafest) leo Jijini Dar es Salaam. Tanzania
inatarajiwa kuwakilishwa na wasanii takribani 240.
Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds
Media Group (CMG), Bw. Ruge Mutahaba akichangia mada wakati wa kikao cha
wanakamati ya maandalizi ya kufanikisha ushiriki wa Tanzania katika
Tamasha la Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki (Jamafest)
litakalofanyika Jijini Kampala, Uganda, leo Jijini Dar es Salaam.
Tanzania inatarajiwa kuwakilishwa na wasanii takribani 240.
Mwakilishi wa Shirika la
Utangazaji la Taifa (TBC), Bw. Nelson Madirisha akisisitiza jambo wakati
wa kikao cha wadau kufanyikisha ushiriki wa Tanzania katika Tamasha la
Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki (Jamafest) litakalofanyika
Jijini Kampala, Uganda, leo Jijini Dar es Salaam. Tanzania inatarajiwa
kuwakilishwa na wasanii takribani 240.
Picha ikionyesha namba
zinazotumika kupokea michango kutoka kwa wadau kwa ajili ya kusaidia
ushiriki wa wasanii kutoka Tanzania katika Tamasha la Utamaduni la
Jumuiya ya Afrika Mashariki (Jamafest) itakayofanyika Jijini Kampala
Uganda mapema mwezi Septemba.
Mmoja wa wadau wa Sanaa na
Utamaduni Bi. Esther Baruti akielezea jambo wakati wa kikao cha wadau
kufanyikisha ushiriki wa Tanzania katika Tamasha la Utamaduni la Jumuiya
ya Afrika Mashariki (Jamafest) litakalofanyika Jijini Kampala, Uganda,
leo Jijini Dar es Salaam. Tanzania inatarajiwa kuwakilishwa na wasanii
takribani 240.
Mmoja wa wadau wa Sanaa na
Utamaduni akijaza fomu baada ya kutoa ahadi ya kuchangia fedha kwa ajili
ya kufanikisha ushiriki wa Tanzania katika Tamasha la Utamaduni la
Jumuiya ya Afrika Mashariki (Jamafest) litakalofanyika Jijini Kampala,
Uganda, katika mkutano uliowakutanisha wanakamati walioteuliwa na Mhe.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison
Mwakyembe (hayupo pichani) leo Jijini Dar es Salaam. Tanzania
inatarajiwa kuwakilishwa na wasanii takribani 240.
Picha na: Frank Shija – MAELEZO
No comments :
Post a Comment