Harry Kane amefunga magoli manne
wakati Tottenham ikitakata na kuichakaza vibaya timu ya Leicester
City kwa magoli 6-1.
Licha ya kupoteza matumaini ya
kutwaa ubingwa wiki iliyopita kikosi hicho kinachonolewa na kocha
Mauricio Pochettino kilihakikisha kinashinda mechi 25 katika msimu
huu.
Katika mchezo huo Kane alifunga
magoli mawili akiwa karibu na goli na magoli mengine mawili akiwa
umbali wa yadi 20 na kufikisha magoli 26 katika msimu huu.
Mkorea Kusini Son Heung-min naye
alifunga magoli mawili mazuri moja katika kila kipindi huku Dele Alli
akifunga baada ya kupatiwa pasi nzuri.
Harry Kane akifunga goli lake la kwanza katika mchezo huo
Son Heung-min akipachika goli la pili la Tottenham
Harry Kane akifunga goli lake la pili katika mchezo huo
No comments :
Post a Comment