Friday, February 23, 2018

VIDEO: NAIBU WAZIRI SUBIRA MGALU AWASHA UMEME KITUO CHA MBAGALA

Kufuatia kuwashwa kwa kituo hicho, Wananchi wa Mbagala ,Kigamboni ,Tandika na Mkuranga na Wenye Viwanda watapata Umeme wenye Nguvu na wenye uhakika ambao hautokatika.
Naibu waziri wa Nishati, amewapongeza wananchi wakazi wa maeneo hayo Kwa kuwa na subira huku akiwapa pole kwa kero ya umeme ya muda Mrefu.
Aidha, alisema amewashukuru Waheshimiwa Wabunge wa Majimbo ya Kigamboni Dk Ndungulile na Mhe Mangungu na Wakuu wa Wilaya Kwa kufuatilia Jitahada za kuondosha Kero hiyo ya Upatikanaji wa Nishati ya Uhakika katika Maeneo hayo.
 
Alisema Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli imefanya juhudi kubwa kutekeleza mradi huo ili wananchi waondokane na kero hiyo.
Alisema kufuatia ushirikiano alionao yeye pamoja na Waziri wa nishati Dk Medard Kalemani wameweza kufanikisha Miradi mbalimbali ya Nishati ya umeme hapa nchini hali inayopelekea wananchi kujenga imani na serikali yao ya awamu ya tano katika utekelezaji wa miradi.
Aliongeza kwa kusema kuwa, kufuatia ushirikiano na Waziri wa nishati, imepelekea kuwa karibu na Wataalam wote wa TANESCO pamoja na Wakandarasi na hatimae kufanikisha mradi huo na miradi mingine iliyo chini ya wizara hiyo.
@ www.habari360.co.tz

No comments :

Post a Comment