Naibu
waziri wa Nishati, amewapongeza wananchi wakazi wa maeneo hayo Kwa kuwa
na subira huku akiwapa pole kwa kero ya umeme ya muda Mrefu.
Aidha,
alisema amewashukuru Waheshimiwa Wabunge wa Majimbo ya Kigamboni Dk
Ndungulile na Mhe Mangungu na Wakuu wa Wilaya Kwa kufuatilia Jitahada za
kuondosha Kero hiyo ya Upatikanaji wa Nishati ya Uhakika katika Maeneo
hayo.
Alisema
Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dk John Pombe Magufuli imefanya juhudi kubwa kutekeleza mradi
huo ili wananchi waondokane na kero hiyo.
Alisema
kufuatia ushirikiano alionao yeye pamoja na Waziri wa nishati Dk Medard
Kalemani wameweza kufanikisha Miradi mbalimbali ya Nishati ya umeme
hapa nchini hali inayopelekea wananchi kujenga imani na serikali yao ya
awamu ya tano katika utekelezaji wa miradi.
Aliongeza
kwa kusema kuwa, kufuatia ushirikiano na Waziri wa nishati, imepelekea
kuwa karibu na Wataalam wote wa TANESCO pamoja na Wakandarasi na hatimae
kufanikisha mradi huo na miradi mingine iliyo chini ya wizara hiyo.
@ www.habari360.co.tz
No comments :
Post a Comment