Wednesday, February 21, 2018

TRA YAWASAJILI WALIPAKODI WAPYA UVINZA,MKOANI KIGOMA


PICHA 1 PICHA 2 PICHA 3 PICHA 4
Kamishna wa Kodi za Ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Elijah Mwandumbya akiongea na Wafanyabiashara wa Wilaya ya Uvinza kuhusu umuhimu wa kupata Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) wakati wa Uzinduzi wa zoezi la uandikishaji wa Walipakodi wapya katika Wilaya hiyo Mkoani Kigoma.
PICHA 5
Baadhi ya Wafanyabiashara wa Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma wakipata maelezo juu ya namna ya kupata Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) toka kwa Kamishna wa Kodi za Ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Elijah Mwandumbya (hayupo pichani) wakati wa Uzinduzi wa zoezi la uandikishaji wa Walipakodi wapya Wilayani hapo.
PICHA 6
Kamishna wa Kodi za Ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Elijah Mwandumbya (aliyekaa) akimsajili Mfanyabiashara wa Wilaya ya Uvinza, Bw. Samson Jacob ili aweze kupata Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) wakati wa Uzinduzi wa zoezi la uandikishaji wa Walipakodi wapya katika Wilaya hiyo Mkoani Kigoma.
PICHA 7.
Kamishna wa Kodi za Ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Elijah Mwandumbya (kulia) akimkabidhi Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) mmoja wa Wafanyabiashara wa Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma mara baada ya kumfanyia usajili.
(PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-TRA
…………………
Na Rachel Mkundai, Kigoma
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeendelea na kampeni yake ya kuwasajili walipakodi wapya katika maeneo mbalimbali nchini na jana zoezi hilo limefanyika katika Wilaya ya Uvinza, mkoani Kigoma.

Zoezi hilo ambalo liliongozwa na Kamishna wa Kodi za Ndani wa TRA Bw. Elijah Mwandumbya ambaye amewataka wakazi wa wilaya ya Uvinza kujitokeza kutumia fursa hiyo ambapo TRA imewafuata kwenye maeneo yao.
“Tunaamini wengine hawajawahi kabisa kupata namba ya utambulisho wa mlipakodi, tumeona ni vema tusogee kwenu ili kama kuna mambo ambayo hamyaelewi mtuulize tuweze kuwafafanulia, lakini ya ambao tumeijia hapa ni kuja kuwasajili na kuwapatia namba ya utambulisho wa mlipakodi”, amesema Bw. Mwandumbya.
Aidha, ameongeza kuwa ili kutimiza lengo na mikakati mbalimbali ya serikali katika kuwahudumia wananchi lazima kodi ikusanywe na hivyo amewasihi wananchi wa Uvinza kujitokeza kujisajili na kulipa kodi stahiki kwa mujibu wa sheria za kodi.
Naye Afisa biashara wa wilaya ya Uvinza Bw. Godfrey Celestine amesema, hii ni fursa na neema kwa wakazi wa wilaya hiyo kwa kuwa upatikanaji wa namba ya utambulisho wa mlipakodi utasaidia wafanyabiashara kupata leseni za biashara kwa urahisi na kurahisisha ufanyaji biashara na kulipakodi stahiki kwa serikali.
“Zoezi hili litawasaidia siyo tu kupata namba ya utambulisho ya mkipakodi bali pia kupata cheti safi cha kodi (tax clearance certificate) ambayo itawawezesha kupata leseni kwa urahisi, nawasihi watumie fursa hii waweze kufanya biashara zao kwa uhuru na kulipakodi”,  
Nao wafanyabishara wameeleza furaha yao kwa TRA kuwafuata mahali walipo na kuwasajili kuwa walipakodi na wamesema kwa sasa wanajua umuhimu wa kulipakodi kwa kuwa wanaona maendeleo yanayotokana na kodi hizo.
Mmoja wa wananchi hao Bw. Hamis Lugoe amesema “Ni wajibu wa wafanyabishara kulipa kodi kwa kuwa kodi ndiyo inaleta maendeleo na kuboresha maisha kwa wananchi wote hata wa vijijini”, alisema.     
Mfanyabishara mwingine aliyefika kusajiliwa Bi. Milembe Almas amesema amewasihi wafanyabiashara wengine kupenda kupata elimu ya kodi kabla ya kwenda kulipa kodi ili waelewe kama yeye alivyoelewa umuhimu wa kulipakodi kwa maendeleo ya taifa.
Kabla ya kuwasajili, Kamishna wa kodi za ndani, Bw. Mwandumbya alipata fursa ya kuwapa elimu ya kodi wakazi wa eneo la senta katika wilaya ya Uvinza na wananchi walipata fursa ya kuuliza maswali mbalimbali na kupata ufafanuzi wa kina

No comments :

Post a Comment