Naibu
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Abdalla Ulega akiteketeza nyavu haramu
zilizounganishwa 21710 zenye macho madogo,makokolo ya Sangara 695,Timba
690,makokoro ya dagaa 90 wilayani Chato.
Mkuu wa Wilaya Chato,Shaban Ntalambe akishiriki zowezi la akiteketeza nyavu haramu .
Naibu
waziri wa Mifungo na Uvuvi Mhe.Abdallah Ulega akizungumza na wananchi
wa Mwembeni pamoja na watumishi na viongozi kuacha kuendelea na tabia ya
kushirikiana na wavuvi haramu.
Naibu
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Abdalla Ulega akiwa ameambatana na
Mkuu wa Wilaya chato,Shaban Ntalambe wakielekea katika kisiwa cha
hifadhi ya Lubondo.
Naibu
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Abdalla Ulega akizungumza na Wafanyakazi
wa Hifadhi ya Lubondo juu ya kuacha kushirikiana na wavivu haramu kwani
wamekuwa wakiwaruhusu kuingia kwenye hifadhi na kuwafichia zana zao
wanapomaliza kuvua.
…………………
Na,Alex Sonna,Chato
Naibu waziri wa Mifungo na Uvuvi
Mhe.Abdallah Ulega leo ameteketeza zana haramu katika Ziwa Victoria
zikiwemo Nyavu za Makila zilizounganishwa 21710 zenye macho
madogo,makokolo ya Sangara 695,Timba 690,makokoro ya dagaa 90 pamoja na
Pikipiki tano zilizokuwa zikitumia katika kusafirisha Samaki haramu.
Akizungumza na wananchi wa
Mwembeni Wilayani Chato Mhe.Ulega amewata kushirikiana na Serikali ya
awamu ya tano chini ya Rais Magufuli kuwafichuwa haralifu hao ili waweze
kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kupigwa faini ama kwenda jela.
”Serikali haitamuonea mtu huruma
awe kiongozi au Raia wa kawaida Sheria itachukuwa mkondo wake nia yetu
nikuona Samaki wanaongezaka ziwa Victoria na watu wavue kwa kufuata
sheria ili Taifa liweze kupata mapato pamoja na ajira kwa wananchi
mbalimbali” amesema Mhe.Ulega
Aidha Naibu Waziri huyu amewaonya
Wafanyakazi wa Hifadhi ya Rubondo kuacha tabia ya kupewa rushwana wavivu
haramu kwani wamekuwa wakiwaruhusu kuingia kwenye hifadhi na kuwafichia
zana zao wanapomaliza kuvua na kuwapatia fedha laki mbili hadi tatu.
Hatua hiyo imetokana na oparesheni
ya Kitaifa ya kupambana na uvuvi haramu ambayo inaendelea kwenye maeneo
ya ziwa victoria ikiwa na lengo la kuondoa uvuvi haramu pamoja na
mitandao ya wafanyabiashara wa zana haramu za kuvulia ,biashara ya
samaki wachanga na utoroshaji wa samaki na mazao ya yake,kwenda nje ya
nchi kinyume cha sheria.
Aidha kiongozi wa oparesheni bwana
Gabriel Mageni aliongeza kuwa katika operesheni hiyo ambayo ina siku
kumi na tatu baadhi ya mambo ambayo wameyabaini ni pamoja na baadhi ya
viongozi wa vijiji na maofisa pamoja na Madiwani wanaosimamia maeneo ya
uvuvi kuwapa hifadhi raia wa kigeni wanaofanya shughuli za uvuvi wakiwa
hawana kibali na kusababisha hasara Serikali ikiwemo kukosa mapato
mapato.
mapato.
Wakati huo huo Mkuu wa Wilaya ya Chato ,Shaban Ntalambe
,amewataadhalisha watendaji ambao wanashirikiana na wavuvi haramu kuwa
endapo kuna mtu hakibainika na kitendo hicho serikali itahakikisha
inamchukulia hatua kupitia oparesheni hiyo hatabakia hata mtu mmoja
ambaye anajihusisha na shughuli hizo awe kiongozi Mkubwa ama mtu wa
kawaida.
No comments :
Post a Comment