Tuesday, January 23, 2018

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI ATEKETEZA ZANA ZA UVUVI HARAMU WILAYANI CHATO


????????????????????????????????????
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Abdalla  Ulega  akiteketeza nyavu haramu  zilizounganishwa 21710 zenye macho madogo,makokolo ya Sangara 695,Timba 690,makokoro ya dagaa 90 wilayani Chato.
????????????????????????????????????
Mkuu  wa Wilaya Chato,Shaban Ntalambe akishiriki zowezi la akiteketeza nyavu haramu .
????????????????????????????????????
Naibu waziri wa Mifungo na Uvuvi Mhe.Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa Mwembeni pamoja na watumishi na viongozi kuacha kuendelea na tabia ya kushirikiana na wavuvi haramu.
????????????????????????????????????
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Abdalla  Ulega akiwa ameambatana na  Mkuu  wa Wilaya chato,Shaban Ntalambe wakielekea katika kisiwa cha hifadhi ya Lubondo.
????????????????????????????????????
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Abdalla  Ulega akizungumza na Wafanyakazi wa Hifadhi ya Lubondo juu ya kuacha kushirikiana na wavivu haramu kwani wamekuwa wakiwaruhusu kuingia kwenye hifadhi na kuwafichia zana zao wanapomaliza kuvua.
…………………
Na,Alex Sonna,Chato
Naibu waziri wa Mifungo na Uvuvi Mhe.Abdallah Ulega leo ameteketeza zana haramu katika Ziwa Victoria zikiwemo Nyavu za Makila zilizounganishwa 21710 zenye macho madogo,makokolo ya Sangara 695,Timba 690,makokoro ya dagaa 90 pamoja na Pikipiki tano zilizokuwa zikitumia katika kusafirisha Samaki haramu.

Akizungumza na wananchi wa Mwembeni Wilayani Chato Mhe.Ulega amewata kushirikiana na Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli kuwafichuwa haralifu hao ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kupigwa faini ama kwenda jela.
”Serikali haitamuonea mtu huruma awe kiongozi au Raia wa kawaida Sheria itachukuwa mkondo wake nia yetu nikuona Samaki wanaongezaka ziwa Victoria na watu wavue kwa kufuata sheria ili Taifa liweze kupata mapato pamoja na ajira kwa wananchi mbalimbali” amesema Mhe.Ulega
Aidha Naibu Waziri huyu amewaonya Wafanyakazi wa Hifadhi ya Rubondo kuacha tabia ya kupewa rushwana wavivu haramu kwani wamekuwa wakiwaruhusu kuingia kwenye hifadhi na kuwafichia zana zao wanapomaliza kuvua na kuwapatia fedha laki mbili hadi tatu.
Hatua hiyo imetokana na oparesheni ya Kitaifa ya kupambana na uvuvi haramu ambayo inaendelea kwenye maeneo ya ziwa victoria ikiwa na lengo la kuondoa uvuvi  haramu pamoja na  mitandao ya wafanyabiashara wa zana haramu za kuvulia ,biashara ya samaki wachanga na utoroshaji wa samaki na mazao ya yake,kwenda nje ya nchi kinyume cha sheria.
Aidha kiongozi wa oparesheni bwana Gabriel Mageni aliongeza kuwa  katika operesheni hiyo ambayo ina siku kumi na tatu baadhi ya mambo ambayo wameyabaini ni pamoja na  baadhi ya viongozi wa vijiji na maofisa pamoja na Madiwani wanaosimamia maeneo ya uvuvi kuwapa hifadhi raia wa kigeni  wanaofanya shughuli za uvuvi wakiwa hawana kibali na kusababisha hasara Serikali ikiwemo kukosa mapato
mapato.
Wakati huo huo Mkuu wa Wilaya ya Chato  ,Shaban Ntalambe ,amewataadhalisha  watendaji ambao wanashirikiana na wavuvi haramu kuwa endapo kuna mtu hakibainika na kitendo hicho serikali itahakikisha inamchukulia hatua kupitia oparesheni hiyo hatabakia hata mtu mmoja ambaye anajihusisha na shughuli hizo awe kiongozi Mkubwa ama mtu wa kawaida.

No comments :

Post a Comment