Friday, November 24, 2017

ROBINHO AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA TISA JELA KWA UBAKAJI

Mchezaji soka wa Brazil Robinho amehukumiwa kifungo cha miaka tisa jela kwa kuhusika katika tukio la ubakaji lililohusisha kundi la wanaume huko Milan nchini Italia mnamo mwaka 2013.

Mahakama ya nchini Italia imetoa huku kwa mchezaji huyo mwenye miaka 33 na wenzake watano raia wa Brazil kwa kumbaka mwanamke raia wa Albainia aliyekuwa na miaka 22 wakati huo baada ya kumlewesha kwenye klabu ya usiku.

Mshambuliaji huyo aliondoka AC Milan mwaka 2015 baada ya kuitumikia kwa miaka mitano na wakati hukumu hiyo ikitolewa hakuwepo Mahakamani na alikanusha shtaka hilo kupitia kwa wakili wake.
Hata hivyo Robinho hataanza kutumikia kifungo hicho kwanza hadi hapo rufaa yake ya hukumu hiyo itakaposikilizwa.

No comments :

Post a Comment