Mwenyekiti wa bodi ya mfuko wa GEPF
Joyce Shaidi akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi millioni 500
kwa Meneja wa Chama cha Kuweka na Kukopa cha Sukari mkoani Kagera Robert Mshoki
Na
CHRISTIAN GAYA, MTANZANIA, ALHAMISI OKTOBA 19, 2017
Takwimu
zilizotolewa mwaka 2012 zinaonesha ya kuwa ni watu
milioni 1.7 tu ndio waliojiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii wakati idadi ya
watanzania wote ni milioni 44.9 hii ikiwa ni asilimia 6.5 tu ya nguvu kazi yote
ya watu milioni 23.7.
Pia pensheni zinazotolewa na mifuko iliyopo hapa nchini hazitoshelezi mahitaji
ya watanzania wakiwemo wastaafu na
familia zao.
Hifadhi ya Jamii ni haki ya kila Mtanzania. Haki hii imeanishwa wazi katika Katiba ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 11(1) na Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2003.
Haki
hii pia imeiainishwa kwenye mkataba wa kimataifa wa haki za binadamu wa mwaka
1948 pamoja na mikataba ya shirika la kazi duniani (ILO) ibara ya 102 ya mwaka
1952.
Na
ndiyo maana Mfuko wa Mafao ya Kustaafu GEPF mwaka 2009 walianzisha mpango wa hiari
wa kujiwekea akiba ya uzeeni kwa lengo la kuwawezesha watu wote wenye uwezo wa
kuzalisha kipato kujiwekea akiba ili kuwasaidia kutimiza malengo yao katika
maisha kama vile kuanzisha au kukuza biashara, matibabu, ujenzi, kulipa ada za
shule na kukabiliana na majanga mbali mbali, hasa pale uwezo au nguvu ya
kuzalisha kipato inapopungua.
Majanga
yapo ya aina nyingi kama vile moto, mafuriko, ukame, ajali na magonjwa mbali
mbali yanayosababisha binadamu asiweze kukabiliana nayo kwa haraka pindi
yanapotokea.
Mtu
yeyote mwenye uwezo wa kuzalisha kipato anaweza kujiunga na mpango huu, awe ameajiriwa
na anachangia kwenye mfuko wowote wa hifadhi ya jamii au amejiajiri mwenyewe
kama vile; Mkulima, Mvuvi, Mama Lishe, Dereva boda boda, Mjasiriamali
yoyote. Kujiunga na mpango huu wa kujiwekea akiba ya uzeeni ni bure
Kiwango
chochote kinaruhusiwa kuanza kujiwekea akiba kulingana na uwezo wa mwanachama.
Mwanachama anaweza kuweka akiba wakati wowote, iwe kila siku, kila wiki, kila
mwezi au kwa msimu.
Mwanachama anaweza kujiwekea akiba kwa kwa njia ya Simu ya Kiganjani (M-pesa, Tigo pesa au Airtel Money), benki
kama vile CRDB, NMB, NBC au benki yoyote mwanachama anakotunza fedha zake, Mawakala
waliothibitishwa na GEPF, Kuwasilisha moja kwa moja kwenye Ofisi za Mfuko
wa GEPF zilizo Mikoani au Makao Makuu.
Wanachama
wa mpango wa hiari wa kujiwekea akiba hulipwa riba kutokana na michango yao.
Wengi wa wanachama hawa hawakidhi vigezo vya kulipwa pensheni hivyo wanasalia
katika utaratibu wa akiba. Pamoja na wanachama wa mpango wa hiari kuna
baadhi ya wanachama walioko katika mpango wa lazima ambao hawatakidhi kulipwa
pensheni hivyo nao pia watalipwa michango yao pamoja na riba. Kwa sasa Mfuko
unatoa riba ya 7.5%. Kiasi hiki
kinatolewa ili kulinda thamani ya michango ya wanachama.
Faida za kujiunga na Mpango wa Hiari wa kujiwekea
Akiba ya Uzeeni,ni kwamba hakuna gharama yoyote inayotozwa
wakati wa kuweka akiba, gawio kubwa la mapato linaloongezeka kila mwaka
linalotokana na uwekezaji kwenye vitega uchumi mbali mbali, mwanachama anaweza
kuchukua sehemu ya akiba yake wakati wowote wa dharura bila kutozwa fedha
yoyote, kupata malipo bila usumbufu ndani ya siku saba za kazi, michango ya
mwanachama inamuwezesha kulipwa pensheni endapo ataweka kiasi na muda unaofuzu
vigezo vya kulipwa pensheni, mikopo kupitia SACCOS au vikundi vilivyojisajili
vya wanachama, kupatiwa pembejeo za kilimo kwa wakulima wanaozalisha kwa wingi.
Mwandishi wa makala hii ni mwanzilishi wa Kituo cha
HakiPensheni, mshauri na mtaalamu wa masuala ya pensheni. Kwa maelezo zaidi gayagmc@yahoo.com unaweza kutembelea
tovuti hakipensheni monitor
online na hakipensheni blog Simu +255 655 13
13 41
No comments :
Post a Comment