Friday, September 22, 2017

TAMASHA LA TULIA TRUST LAPAMBA MOTO TUKUYU


01
Nahodha wa timu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi iliyoundwa na wachezaji kutoka kutoka Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uhamiaji Amina Juma Kizaba akipokea kombe la ushindi wa kwanza kutoka kwa Mdadhimu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Luteni Jenerali James A. Mwakibolwa jana Tukuyu Mbeya baada ya kuilaza timu pinzani ya Kiimo Kijiji Kitulivu (KKR) kwa mabao 26-16.
02
Baadhi ya wachezaji wa timu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi iliyoundwa na wachezaji kutoka kutoka Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uhamiaji wakifurahia ubingwa wao mara baada ya mechi jana Tukuyu Mkoani Mbeya.
03
Wachezaji wa timu ya Ndato wakifanya mazoezi kabla ya mechi yao dhidi ya timu ya Isange.
04
Wachezaji wa timu ya Ndato (waliovaa jezi nyeupe) wakimenyanya na timu ya Isange (waliovaa jezi za bluu) wakati wafainali ya Tamasha la Tulia Trust Tukuyu mkoani Mbeya.
Picha na Eleuteri Mangi,WHUSM, Tukuyu
………………………
Na Eleuteri Mangi, WHUSM, Tukuyu.
Washindi wa mchezo wa soka na mpira wa pete wapokea kitita cha wamepokea kitika cha Sh. 7,500,000/= katika Tamasha la Ngoma za ...
Jadi linaloratibiwa na Taasisi ya Tulia Trut wilayani Tukuyu mkoa wa Mbeya.
Tamasha hilo limeifanya wilaya ya Tukuyu kuendelea kung’ara katika tasnia ya michezo kwa kupambwa na michezo mbalimbali ikiwemo soka, mpira wa pete na ngoma za jadi ambapo tamasha hilo linatarajiwa kuhitimishwa Septemba 23 mwaka huu na kuongozwa na kaulimbiu “Tuuenzi Utamaduni wetu”.
Uwanja wa Tulia ambao awali ulikuwa unaitwa Tandale ulifurika mashabiki kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa huo na mikoa inayoshiriki tamasha hilo wameshuhudia timu za Ndato na Isange zilipokutana kumenyana katika hatua ya fainali ambapo Ndato ndio walioibuka kidedea kwa kuwalaza Isange kwa mabao 2-1.
Mchezo huo ulianza kwa kasi huku kila timu ikitafuta bao la mapema ambapo dakika ya pili kipindi cha kwanza Ndato ndio waliofanikiwa kupata bao la kuongoza lililofungwa na mchezaji Monte Stephano.
Mashambulizi ya kushtukiza yaliendelea kwa kila upande ili kutafuta ushindi, dakika ya 18 kipindi cha kwanza Isange walipata bao la kusawazisha kupitia kapteni wake Hussein Mwalugaja, bao lililozipeleka timu zote kwenye mapumziko kwa kufungana    goli 1-1.
Kipindi cha pili kilianza kwa vuta nikuvute ambapo Ndato ndio walifanikiwa kupata bao la kuongoza ambapo hadi kipenga cha mwisho Ndato ndio walioibuka kidedea kwa mabao 2-1.
Kwa upande wa mpira wa pete, timu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi iliyoundwa na wachezaji kutoka kutoka Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto na Uhamiaji waliwalaza timu pinzani ya Kiimo Kijiji Kitulivu (KKR) kwa mabao 26-16.
Kwa ushindi huo, bingwa ambao ni timu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imepata zawadi ya kombe, medali na kujipatia kitita cha Sh. 1,500,000/= wakati mshindi wa pili ambaye ni timu ya KKR nayo ikijipatia kombe, medali na kitita cha Sh. 1000,000/=  huku mshindi wa tatu akijipatia sh. 750,000/= na mshindi wa nne akiweka kibindoni sh.500,000/=
Akizungumzia tamasha hilo linaloendelea hadi Sptemba 23 mwaka huu, Mwasisi wa Taasisi ya Tulia Trust ambaye pia ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson amesema kuwa wamejipanga kulifanya tamasha hilo kuwa endelevu na kuwa na wigo mpana zaidi na hatimaye kufikia nchi nzima.
Dkt. Tulia Ackson amewashukuru wadhamini kwa kufanikisha tamasha hilo na kuwa waomba waendelee kujitoa kwa lengo la kuijenga Tanzania yenye utamaduni imara unaotoa ajira na kulinda maadili ya Kitanzania.
Wadhamini hao ni pamoja na Benki ya CRDB, Ubalozi wa China, Umoja wa  Mataifa (UN), Ubalozi wa Ujerumani, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Bodi ya Utalii Tanzania, PPF, WCF, Vodacom, TCRA, pamoja na Kampuni ya TOL Gas Ltd.

No comments :

Post a Comment